Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo sauti-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo sauti-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote

Jumatatu, 30 Septemba 2019

2. Kujua madhumuni na Umuhimu wa Kila Moja ya Hatua Tatu za Kazi ya Mungu

II. Ni Lazima Mtu Ashuhudie Kipengele cha Ukweli Kuhusu Hatua Tatu za Kazi ya Wokovu wa Mungu kwa Wanadamu

2. Kujua madhumuni na Umuhimu wa Kila Moja ya Hatua Tatu za Kazi ya Mungu

(1) Lengo na umuhimu wa kazi ya Mungu katika Enzi ya Sheria

Maneno Husika ya Mungu:

    Kazi ambayo Yehova alifanya kwa Waisraeli ilianzisha mahali pa Mungu pa asili miongoni mwa binadamu, ambapo pia palikuwa pahali patakatifu ambapo Alikuwapo. Aliwekea kazi Yake mipaka kwa watu wa Israeli. Mwanzoni, Hakufanya kazi nje ya Israeli; badala yake, Aliwachagua watu Aliowaona kuwa wa kufaa ili kuzuia eneo la kazi Yake. Israeli ni mahali ambapo Mungu aliwaumba Adamu na Hawa, na kutoka katika mavumbi ya mahali hapo Yehova alimuumba mwanadamu; mahali hapa pakawa kituo cha kazi Yake duniani. Waisraeli, ambao walikuwa wa ukoo wa Nuhu na pia wa ukoo wa Adamu, walikuwa msingi wa kibinadamu wa kazi ya Yehova duniani.

Alhamisi, 12 Septemba 2019

Swali la 5: Bwana Yesu alikuwa Mungu mwenye mwili na hakuna yeyote anaweza kukanusha hili. Sasa unashuhudia kwamba Mwenyezi Mungu ni Bwana Yesu aliyerudi katika mwili, lakini wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wanasema kuwa kile unachoamini ni mtu tu, wanasema kuwa umedanganywa, na hatuwezi kulielewa jambo hili. Wakati huo Bwana Yesu alipokuwa mwili na kuja kufanya kazi ya ukombozi, Mafarisayo Wayahudi pia walisema kuwa Bwana Yesu alikuwa mtu tu, wakisema kwamba mtu yeyote aliyemwamini Yeye alikuwa akidanganywa. Kwa hiyo, tungependa kufuatilia kipengele hiki cha ukweli kuhusu kupata mwili. Kupata mwili ni nini hasa? Na ni nini asili ya kupata mwili? Tafadhali shiriki hili kwa ajili yetu.

Jibu:

    Imani yenu katika Bwana Yesu kama kupata mwili kwa Mungu si uwongo. Lakini mbona mnamwamini Bwana Yesu? Je, kweli mnamfikiria Bwana Yesu kuwa ni Mungu? Mnamwamini Bwana Yesu kwa sababu ya kile kilichorekodiwa katika Biblia na kwa sababu ya kazi ya Roho Mtakatifu. Lakini haijalishi mnachosema, ikiwa hamjamwona Bwana Yesu uso kwa uso, je, mwaweza kuthubutu kusema kwamba mnamjua Bwana Yesu? Katika imani yenu kwa Bwana, mnarudia tu maneno ya Petro, aliyesema kwamba Bwana Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu aishiye, lakini je, mnaamini kwamba Bwana Yesu ni dhihirisho la Mungu,

Jumatano, 3 Julai 2019

Matamshi ya Mungu | “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I” Sehemu ya Kwanza

Sauti ya Mungu | “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I” Sehemu ya Kwanza

Mwenyezi Mungu anasema, “Tabia ya Mungu iko wazi kwa kila mmoja na haijafichwa, kwa sababu Mungu hajawahi kuepuka kimakusudi mtu yeyote na Hajawahi kimakusudi kujaribu kujificha Mwenyewe ili watu wasiweze kumjua Yeye au kumwelewa Yeye. Tabia ya Mungu siku zote imekuwa wazi na siku zote imekuwa ikitazama kila mtu kwa njia ya uwazi. Katika usimamizi wa Mungu,

Jumamosi, 15 Juni 2019

3. Kwa nini ukweli unaoonyeshwa na Mungu katika siku za mwisho unaweza kumtakasa mtu, kumkamilisha mwanadamu na kuwa maisha ya mwanadamu?

XVII. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Jinsi ya Kutambua Kati ya Uhalisi wa Ukweli na Maarifa ya Biblia na Mafundisho
3. Kwa nini ukweli unaoonyeshwa na Mungu katika siku za mwisho unaweza kumtakasa mtu, kumkamilisha mwanadamu na kuwa maisha ya mwanadamu?
Maneno Husika ya Mungu:

Njia ya maisha si kitu ambacho kinaweza kumilikiwa na mtu yeyote tu, wala hakipatikani kwa urahisi na wote. Hiyo ni kwa sababu maisha yanaweza kuja tu kutoka kwa Mungu, ambayo ni kusema, Mungu Mwenyewe tu ndiye Anamiliki mali ya maisha, hakuna njia ya maisha bila Mungu Mwenyewe, na hivyo Mungu tu ndiye chanzo cha uzima, na kijito cha maji ya uzima kinachotiririka nyakati zote. Kutoka Alipoumba dunia, Mungu amefanya kazi kubwa inayoshirikisha uhai wa maisha, Amefanya kazi kubwa ambayo huletea mwanadamu maisha, na Amelipa gharama kubwa ili mtu aweze kupata uzima, kwa kuwa Mungu Mwenyewe ni uzima wa milele, na Mungu Mwenyewe ni njia ambayo kwayo mtu hufufuliwa. Mungu kamwe hajawahi kosa kwa moyo wa mwanadamu, na Anaishi miongoni mwa binadamu wakati wote. Amekuwa nguvu ya kuendesha maisha ya mwanadamu, chanzo cha kuwepo kwa binadamu, na amana ya fahari ya kuwepo kwa binadamu baada ya kuzaliwa. Husababisha binadamu kuzaliwa upya, na kumwezesha kwa ushupavu kuishi kwa kila jukumu lake. Kwa sababu ya uwezo Wake, na nguvu ya maisha Yake yasiyopungua, binadamu ameishi kwa kizazi baada ya kizazi, ambapo nguvu ya uhai wa Mungu umekuwa uti wa mgongo wa kuwepo kwa binadamu, na ambayo Mungu amelipia gharama ambayo hakuna mtu wa kawaida amewahi kulipa. Nguvu za Mungu za maisha zinaweza kutawala juu ya nguvu zozote; zaidi ya hayo, inazidi mamlaka yoyote. Maisha Yake ni ya milele, nguvu zake za ajabu, na nguvu Zake za maisha si rahisi kuzidiwa na kiumbe yeyote au nguvu za adui. Nguvu za maisha ya Mungu zipo, na hung’aa mwangaza wake ulio mzuri sana, bila ya kujali muda au mahali. Maisha ya Mungu, huishi milele bila kubadilika katika kusumbuka kwa mbingu na nchi. Mambo yote hupita, lakini maisha ya Mungu hubaki, kwa maana Mungu ni chanzo cha kuwepo kwa mambo yote, na mizizi ya kuwepo kwao. Asili ya maisha ya mwanadamu hutoka kwa Mungu, kuwepo kwa mbingu ni kwa sababu ya Mungu, na kuwepo kwa ardhi kunatokana na nguvu ya uhai wa Mungu. Hakuna kitu kinachomiliki nguvu kinachoweza kuzidi ukuu wa Mungu, na hakuna kitu chenye nguvu kinachoweza kuvunja mipaka ya mamlaka ya Mungu. Kwa njia hii, bila kujali wao ni nani, kila mtu lazima ajiwasilishe kwa utawala wa Mungu, kila mtu lazima aishi chini ya amri za Mungu, na hakuna mtu anayeweza kutoroka kutoka katika utawala Wake.

Jumapili, 9 Juni 2019

1. Unyakuo ni lazima utegemezwe maneno ya Mungu na sio dhana na mawazo ya mwanadamu

XX. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Unyakuo ni nini na Maana Halisi ya Kuinuliwa Mbele ya Kiti cha Enzi cha Mungu

1. Unyakuo ni lazima utegemezwe maneno ya Mungu na sio dhana na mawazo ya mwanadamu

Aya za Biblia za Kurejelea:

“Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako ufike, Mapenzi yako yafanywe duniani, kama ilivyo mbinguni” (Mathayo 6:9-10).


“Na mimi Yohana nikauona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukija chini kutoka kwa Mungu mbinguni…. Tazama, hema takatifu la Mungu liko pamoja nao watu, na yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Na yeye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, na kuwa Mungu wao” (Ufunuo 21:2-3).

Jumamosi, 1 Juni 2019

Sauti ya Mungu | “Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja” Sehemu ya Pili


Sauti ya Mungu | “Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja” Sehemu ya Pili
Mwenyezi Mungu anasema, “Mungu aliumba binadamu na Akawaweka duniani, ambao Amewaongoza mpaka siku ya leo. Kisha Akaokoa binadamu na kuhudumu kama sadaka ya dhambi kwa binadamu. Mwishowe lazima bado ashinde binadamu, aokoe binadamu kabisa na kuwarejesha kwa mfano wao wa awali. Hii ndiyo kazi Amekuwa akifanya kutoka mwanzo hadi mwisho—kurejesha mwanadamu kwa sura yake halisi na kwa mfano wake wa awali. Ataanzisha ufalme Wake na kurejesha mfano wa awali wa mwanadamu, kumaanisha kwamba Atarejesha mamlaka Yake duniani na kurejesha mamlaka Yake miongoni mwa viumbe vyote. ... Wakati binadamu wamerejeshwa katika mfano wake wa awali, wakati binadamu wanaweza kutimiza kazi yao husika, kuwa na nafasi zao wenyewe na kutii mipango yote ya Mungu, Mungu atakuwa amepata kundi la watu duniani wanaomwabudu, na Atakuwa pia Ameanzisha ufalme duniani unaomwabudu. Atakuwa na ushindi wa milele duniani, na wale wanaompinga wataangamia milele. Hii itarejesha nia Yake ya asili ya kumuumba mwanadamu; itarejesha nia Yake ya kuumba vitu vyote, na pia itarejesha mamlaka Yake duniani, mamlaka Yake miongoni mwa vitu vyote na mamlaka yake miongoni mwa adui Zake. Hizi ni ishara za ushindi Wake wote. Tangu sasa na kwendelea binadamu wataingia katika raha na kuingia katika maisha yafuatayo njia sahihi. Mungu pia ataingia katika raha ya milele na mwanadamu na kuingia katika maisha ya milele yanayoshirikisha Mungu na mwanadamu. Uchafu na kutotii duniani vitatoweka, na pia maombolezo duniani. Wote walio duniani wanaompinga Mungu hawatakuweko. Mungu na wale Aliowaokoa pekee ndio watabaki; viumbe Wake tu ndio watabaki.”

Kuhusu Sisi:Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu

Jumapili, 24 Machi 2019

Matamshi ya Mungu | “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III” Sehemu ya Sita

Matamshi ya Mungu | “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III” Sehemu ya Sita

Mwenyezi Mungu anasema, “Namna ambavyo Mungu anawatendea watu wanaomkufuru au hata wanaompinga, au hata wale wanaomkashifu—watu wanaomshambulia kimakusudi, kumkashifu, na kumlaani—hajifanyi kwamba kila kitu kiko sawa. Anao mwelekeo wazi kwa hawa. Anawadharau watu hawa, na moyoni Mwake anawashutumu. Anatangaza waziwazi hata matokeo kwa ajili yao, ili watu waweze kujua kwamba Anao mwelekeo wazi kwao wanaomkufuru Yeye, na ili wajue namna atakavyoamua matokeo yao. 

Ijumaa, 22 Machi 2019

Matamshi ya Mungu | Sura ya 97

Matamshi ya  Mungu | Sura ya 97

Mwenyezi Mungu alisema, Nitafanya kila mtu aone matendo Yangu ya ajabu na kusikia maneno Yangu ya hekima. Ni lazima iwe kila mtu na ni lazima iwe juu ya kila suala. Hii ni amri Yangu ya utawala na ni ghadhabu Yangu. Nitahusisha kila mtu na kila jambo ili watu wote kutoka mwisho mmoja wa ulimwengu hadi mwingine wataona kwa macho yao wenyewe, la sivyo Sitaacha kamwe. Ghadhabu Yangu imemwagwa kikamilifu na hakuna hata chembe imezuiwa.

Jumatatu, 18 Machi 2019

maneno ya Mungu | Sura ya 12

maneno ya Mungu | Sura ya 12

Mwenyezi Mungu alisema, Watu wote wanapotilia maanani, wakati vitu vyote vinafanywa upya na kuhuishwa, wakati kila mtu anamtii Mungu bila shaka, na yuko tayari kubeba jukumu zito la mzigo wa Mungu—hapa ndipo wakati umeme wa mashariki unatoka, ukiangaza yote kutoka Mashariki hadi Magharibi, ukiyatisha yote ya ulimwengu na ujaji wa mwanga huu; na wakati huu, Mungu tena huanza maisha Yake mapya.

Jumatatu, 11 Machi 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Saba

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Saba

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”.
Maudhui ya video hii:
Hakuna Anayeweza Kubadilisha Hoja Kwamba Mungu Anashikilia Ukuu juu ya Hatima ya Binadamu
Mtazamo na Matendo Bora ya Mtu Anayependa Kujinyenyekeza katika Mamlaka ya Mungu

Jumatatu, 25 Februari 2019

"Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)" Sehemu ya Kwanza

"Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)" Sehemu ya Kwanza

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”.
Maudhui ya video hii:
Jinsi Mungu Anavyotawala na Kuongoza Ulimwengu wa Kiroho
1. Mzunguko wa Uhai na Mauti wa Wasioamini

Ijumaa, 11 Januari 2019

Neno la Mungu | "Maana ya Kuwa Mwanaadamu Halisi" (Official Video)

Neno la Mungu | "Maana ya Kuwa Mwanaadamu Halisi" (Official Video)

Mwenyezi Mungu anasema, "Hata hivyo unapaswa kujua, wanadamu Nilioumba walikuwa watu watakatifu na wenye mfano Wangu na utukufu Wangu. Hapo awali hawakuwa wa Shetani, wala hawakukabiliwa na kukanyagwa kwake, bali walikuwa tu udhihirisho Wangu, walikuwa huru kutokana na sumu yake. Hivyo, Naliwajulisha wanadamu wote kwamba Ninataka tu kilichoumbwa na mkono Wangu, Wapendwa Wangu walio watakatifu ambao kamwe hawajawahi kumilikiwa na mwingine yoyote.

Alhamisi, 27 Desemba 2018

Sura ya 24 na 25



Mwenyezi Mungu alisema, Bila kusoma kwa makini, haiwezekani kugundua kitu chochote katika matamko ya siku hizi mbili; kwa kweli, yangepaswa kunenwa kwa siku moja, lakini Mungu aliyagawanya kwa siku mbili. Hiyo ni kusema, matamko ya siku hizi mbili yanaunda moja kamili, lakini ili iwe rahisi kwa watu kuyakubali, Mungu aliyagawanya kwa siku mbili ili kuwapa watu nafasi ya kupumua. Hiyo ndiyo fikira ya Mungu kwa mwanadamu. Katika kazi yote ya Mungu, watu wote hutekeleza kazi zao na wajibu wao mahali pao wenyewe.

Alhamisi, 16 Novemba 2017

Umeme wa Mashariki | Tamko La Nane


Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

   Mwenyezi Mungu alisema: Ufunuo Wangu unapofika kilele chake, na wakati hukumu Yangu inapomalizika, utakuwa wakati ambao watu Wangu wote wanafichuliwa na kufanywa wakamilifu. Nyayo zangu hukanyaga kila pembe ya ulimwengu katika hali ya kutafuta kwa kudumu wale wenye kupendeza nafsi Yangu na wanafaa kwa matumizi Yangu.

Alhamisi, 31 Agosti 2017

Kristo Hufanya Kazi ya Hukumu Kwa Ukweli

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

 Umeme wa Mashariki | Kristo Hufanya Kazi ya Hukumu kwa Ukweli

Mwenyezi Mungu alisema, Kazi ya siku za mwisho ni kutenganisha vitu vyote kulingana na jinsi yavyo, kuhitimisha mpango wa usimamizi wa Mungu, kwa maana muda u karibu na siku ya Mungu imewadia. Mungu huwaleta wote ambao wameingia katika ufalme Wake, yaani, wale wote ambao wamekuwa waaminifu Kwake mpaka mwisho, katika enzi ya Mungu Mwenyewe.

Alhamisi, 24 Agosti 2017

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Unapaswa Kutafuta Njia ya Uwiano na Kristo

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Unapaswa Kutafuta Njia ya Uwiano na Kristo

Mwenyezi Mungu alisema, Nimefanya kazi kubwa miongoni mwa binadamu, na maneno ambayo Nimeeleza wakati huu yamekuwa mengi. Maneno haya ni kwa ajili ya wokovu wa mwanadamu, na yalikuwa yanaeleza ili binadamu aweze kulingana na Mimi. Ilhali Nimewapokea watu wachache tu duniani ambao wanalingana na Mimi, na hivyo Nimesema kwamba binadamu hathamini maneno Yangu, kwa kuwa binadamu halingani na Mimi. Kwa njia hii, kazi ambayo Naifanya sio tu kwa ajili ya mwanadamu aweze kuniabudu;

Jumatatu, 21 Agosti 2017

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Wale Wasiopatana Na Kristo Hakika Ni Wapinzani Wa Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Wale Wasiopatana Na Kristo Hakika Ni Wapinzani Wa Mungu


Watu wote wana tamaa ya kuona uso wa kweli wa Yesu na kutaka kuwa pamoja Naye. Naamini kuwa hakuna mmoja wa ndugu au dada anayeweza kusema kwamba yeye hana nia ya kumwona au kuwa pamoja na Yesu. Kabla ya nyinyi kumwona Yesu, yaani, kabla ya nyinyi kumwona Mungu Aliye kwenye mwili, mtakuwa na mawazo mengi, kwa mfano, kuhusu sura ya Yesu, njia Yake ya kuzungumza, njia Yake ya maisha, na kadhalika. Hata hivyo, wakati mnamwona hasa, mawazo yenu yatabadilika haraka. Ni kwa nini? Je, mnataka kujua? Hata ingawa fikira za mwanadamu hakika haziwezi kupuuzwa, haikubaliki kamwe mwanadamu kubadilisha kiini cha Kristo.

Alhamisi, 17 Agosti 2017

Kanisa la Mwenyezi Mungu | NYENDO ZA MATESO YA KIDINI NCHINI CHINA



Tangu kilipokuja mamlakani katika China Bara mnamo mwaka wa 1949, Chama Cha Kikomunisti cha China kimekuwa hakikomi katika mateso yake kwa imani ya kidini. Kwa wayowayo kimewashika na kuwaua Wakristo, kuwafukuza na kuwadhulumu wamishonari wanaofanya kazi nchini China, wakachukua ngawira na kuchoma nakala nyingi za Biblia, wakafunga kabisa na kubomoa majengo ya kanisa, na bila mafanikio wakajaribu kukomesha makanisa yote ya nyumbani.

Jumanne, 1 Agosti 2017

Umeme wa Mashariki | Kuonekana kwa Mungu Kumeleta Enzi Mpya


Umeme wa Mashariki ,Mwenyezi Mungu,Kanisa la Mwenyezi Mungu


Umeme wa Mashariki | Kuonekana kwa Mungu Kumeleta Enzi Mpya


   Mpango wa Mungu wa miaka elfu sita ya usimamizi unaelekea kikomo, na lango la ufalme limefunguliwa kwa wale ambao wanatafuta kuonekana kwa Mungu. Ndugu wapendwa, mnasubiri nini? Mnatafuta nini? Mnausubiri kuonekana kwa Mungu? Mnazitafuta nyayo za Mungu? Kuonekana kwa Mungu kunatamaniwa sana! Ni vigumu, kiasi gani kupata nyayo za Mungu! Katika enzi kama hii, katika dunia kama hii, lazima tufanye nini ili tushuhudie kuonekana kwa Mungu? Sharti tufanye nini ili tufuate nyayo za Mungu?