Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo unabii. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo unabii. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 27 Desemba 2018

Sura ya 24 na 25



Mwenyezi Mungu alisema, Bila kusoma kwa makini, haiwezekani kugundua kitu chochote katika matamko ya siku hizi mbili; kwa kweli, yangepaswa kunenwa kwa siku moja, lakini Mungu aliyagawanya kwa siku mbili. Hiyo ni kusema, matamko ya siku hizi mbili yanaunda moja kamili, lakini ili iwe rahisi kwa watu kuyakubali, Mungu aliyagawanya kwa siku mbili ili kuwapa watu nafasi ya kupumua. Hiyo ndiyo fikira ya Mungu kwa mwanadamu. Katika kazi yote ya Mungu, watu wote hutekeleza kazi zao na wajibu wao mahali pao wenyewe.