Jumapili, 12 Agosti 2018

Swahili Christian Worship Song "Upendo wa Mungu Hutuleta Karibu Zaidi Pamoja"

Swahili Christian Worship Song "Upendo wa Mungu Hutuleta Karibu Zaidi Pamoja"

Ingawa tumetengwa na maziwa na milima isiyohesabika,
sisi tuko pamoja, bila mipaka kati yetu,
tukiwa na rangi tofauti za ngozi na kuzungumza ndimi tofauti.
Kwa sababu maneno ya Mwenyezi Mungu yanatuita,
tunainulia juu mbele ya kiti cha enzi cha Mungu.

Jumamosi, 11 Agosti 2018

Tamko la Arubaini na Sita

Tamko la Arubaini na Sita

Mwenyezi Mungu alisema, Sijui jinsi watu wanavyoendelea katika kuyafanya maneno Yangu kuwa msingi wa kuweko kwao. Nimehisi wasiwasi kila mara kwa ajili ya majaliwa ya mwanadamu, lakini watu hawaonekani kuwa na fahamu yoyote kuhusu hili—na kutokana na hilo, hawajawahi kuyatilia maanani mambo Yangu, na hawajawahi kukuza kuabudu kokote kwa ajili ya mtazamo Wangu kuhusiana na mwanadamu.

Ijumaa, 10 Agosti 2018

Wimbo za wokovu | “Kwa Kuwa Mungu Anamwokoa Mwanadamu, Atamwokoa Kabisa” | Wema wa Mungu

Wimbo za wokovu | “Kwa Kuwa Mungu Anamwokoa Mwanadamu, Atamwokoa Kabisa” | Wema wa 


I
Kwa kuwa Mungu alimuumba mwanadamu, Atamwongoza;
kwa kuwa Anamwokoa mwanadamu, Atamwokoa na kumpata kabisa;
kwa kuwa anamwongoza mwanadamu, Atamfikisha katika hatima sahihi.
Kwa kuwa Alimuumba mwanadamu na Anamsimamia,
ni lazima awajibikie matarajio na jalaa ya mwanadamu.

Alhamisi, 9 Agosti 2018

Nilifurahia karamu kubwa

Kanisa la Mwenyezi Mungu, upendo wa Mungu, Umeme wa Mashariki

Nilifurahia karamu kubwa

Xinwei    Mkoa wa Zhejiang
Juni 25 na 26 zilikuwa siku zisizohaulika. Eneo letu la Zhejiang lilipata tukio kubwa, viongozi wengi na wafanyakazi wa eneo wakiwa wamekamatwa na joka kubwa jekundu. Ni wachache wetu tu tuliokimbia bila kuumia na, mioyo yetu ikiwa imejaa shukrani, tulikula kiapo cha siri kwa Mungu: kushirikiana vizuri na kazi iliyokuwa ifuate. Kufuatia hilo tulianza kazi yenye msisimko na shughuli nyingi ya kushughulika na matokeo. Na baada ya karibu mwezi mmoja, mipango ilikuwa inakaribia kukamilika.

Jumatano, 8 Agosti 2018

"Fichua Siri Kuhusu Biblia" (6) - Je, Bado Tunaweza Kupata Uzima Tukiondoka Kwa Biblia?


"Fichua Siri Kuhusu Biblia" (6) - Je, Bado Tunaweza Kupata Uzima Tukiondoka Kwa Biblia?

    Mara kwa mara wachungaji na wazee huwafundisha watu kuwa hawawezi kuitwa waumini wakiondoka kwenye Biblia, na kwamba kwa kushikilia Biblia pekee ndiyo wanaweza kupata uzima na kuingia katika ufalme wa mbinguni. Kwa hivyo, je, kweli hatuwezi kupata uzima tukiondoka kwenye Biblia? Je, ni Biblia ambayo inaweza kutupa uzima, au ni Mungu ambaye anaweza kutupa uzima?

Jumanne, 7 Agosti 2018

"Fichua Siri Kuhusu Biblia" (2) - Imefichuliwa: Uhusiano Kati ya Mungu na Biblia


"Fichua Siri Kuhusu Biblia" (2) - Imefichuliwa: Uhusiano Kati ya Mungu na Biblia


    Wachungaji na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa dini wanaamini kuwa maneno na kazi zote za Mungu yamo ndani ya Biblia, kwamba wokovu wa Mungu katika Biblia ni mkamilifu na mradi watu waweke msingi wa imani yao katika Bwana katika Bibilia na washikilie Bibilia, basi wanaweza kunyakuliwa na wanaweza kuingia katika ufalme wa mbinguni. Je, kweli ukweli uko namna hii? Je, ni Mungu ambaye anaweza kufanya kazi kutuokoa, au Biblia? Je, ni Mungu ambaye anaweza kuonyesha ukweli, au Biblia? Ili kujifunza zaidi, tafadhali angalia video hii!



    Tazama zaidi:Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumatatu, 6 Agosti 2018

Sinema za Injili "Kutoka kwa Enzi Hububujika Maji ya Uzima" | Roho wa Ukweli Amekuja!

Sinema za Injili "Kutoka kwa Enzi Hububujika Maji ya Uzima" | Roho wa Ukweli Amekuja!

Tao Wei alikuwa mhubiri kutoka kanisa la nyumba. Kanisa lake lilipokuwa na ukiwa zaidi na zaidi siku baada ya siku, wafuasi wake wote wakawa walegevu na wenye roho dhaifu, na roho yake mwenyewe ilikuwa na giza. Yeye hakuweza tena kuhisi uwepo wa Bwana, na Tao Wei alichanganyikiwa, bila kujua la kufanya.