Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kurudi-kwa-Yesu-mara-ya pili. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kurudi-kwa-Yesu-mara-ya pili. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 19 Juni 2019

2. Kwa nini inasemekana kwamba “Utatu” ni kauli ya upuuzi zaidi?

XVI. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kama Mungu Kweli ni Mungu wa Utatu au ni Mungu Mmoja wa Kweli
2. Kwa nini inasemekana kwamba “Utatu” ni kauli ya upuuzi zaidi?
Maneno Husika ya Mungu:
Baada ya ukweli wa Yesu aliyepata mwili kutokea, mwanadamu aliamini hili: Si Baba pekee aliye mbinguni, bali pia Mwana, na hata Roho Mtakatifu. Hii ndiyo dhana ya kawaida aliyonayo mwanadamu, kwamba kuna Mungu wa aina hii mbinguni: Utatu ambao ni Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, wote katika nafsi moja. Wanadamu wote wana fikra hizi: Mungu ni Mungu mmoja, ila Anajumuisha sehemu tatu, kile ambacho wale wote waliofungwa kwa huzuni katika hizi dhana za kawaida wanachukulia kuwa kuna Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Ni sehemu hizo tatu pekee ambazo zimefanywa moja ambazo ni Mungu kamili. Bila Baba Mtakatifu, Mungu asingekuwa mkamilifu. Vivyo hivyo, wala Mungu asingekuwa mkamilifu bila Mwana au Roho Mtakatifu. Katika mawazo yao, wanaamini kuwa Baba au Mwana pekee hawezi kuwa Mungu. Ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu tu kwa pamoja wanaoweza kuwa Mungu Mwenyewe. … Kwa karne nyingi, mwanadamu ameamini katika huu Utatu, ambao umebuniwa na mawazo katika akili za mwanadamu, ukatengenezwa na mwanadamu, na ambao haujawahi kuonekana na mwanadamu. Kwa miaka mingi, kumekuwa na watu maarufu wa kiroho ambao wameeleza “maana ya kweli” ya Utatu, ila maelezo hayo ya Utatu kama nafsi tatu dhahiri yamekuwa si yakini na hayapo wazi na watu wote wamepumbazwa na “ujenzi” wa Mungu. Hakuna mtu maarufu yeyote aliyewahi kutoa maelezo kamili; maelezo mengi yanafaa katika masuala ya mjadala na katika maandishi, ila hakuna hata mtu mmoja ambaye ana ufahamu kamili na wa wazi kuhusu maana ya Utatu. Hii ni kwa sababu huu Utatu huu mkuu ambao mwanadamu anashikilia moyoni kwa hakika haupo.

Jumapili, 16 Juni 2019

2. Matokeo yatakuwa gani kama mtu anamwamini Mungu kwa kutegemea maarifa ya teolojia katika Biblia?

XVII. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Jinsi ya Kutambua Kati ya Uhalisi wa Ukweli na Maarifa ya Biblia na Mafundisho
2. Matokeo yatakuwa gani kama mtu anamwamini Mungu kwa kutegemea maarifa ya teolojia katika Biblia?
Aya za Biblia za Kurejelea:

“Watu hawa wananikaribia kwa vinywa vyao, na wananiheshimu kwa midomo yao; lakini moyo wao uko mbali nami. Lakini wananiabudu bure, wakifunza mafundisho ya dini ambayo ni amri za wanadamu” (Mathayo 15:8-9).

“Kwa sababu andiko huua, lakini roho hupeana maisha” (2 Wakorintho 3:6).