Jumatatu, 27 Mei 2019

Wimbo Mpya wa Dini 2019 | “Zingatia Majaliwa ya Binadamu” | Wokovu wa Mungu (Lyrics Video)

Wimbo Mpya wa Dini 2019 | “Zingatia Majaliwa ya Binadamu” | Wokovu wa Mungu (Lyrics Video) 

Mungu awahimiza makabila yote, 
mataifa na nyanja zote: 
Sikizeni sauti Yake, muione kazi Yake; 
mzingatie hatima ya wanadamu; 
mfanye Mungu Mtakatifu na Mheshimiwa, 
Mkuu na wa pekee wakuabudiwa, 
ulimwengu wote, na wanadamu, 
waishi chini ya baraka Yake Mungu
kama vizazi vya Ibrahimu, 
walivyoishi na ahadi ya Yehova, 
kama viumbe vya Mungu, Adamu na Hawa, 
walivyoishi bustani Edeni. 

Jumapili, 26 Mei 2019

Ushuhuda wa Injili | Upendo wa Mungu ni wa Kweli Kabisa


Wenzhong , Beijing
Agosti 11, mwaka wa 2012
Usiku wa Julai 21, mwaka wa 2012, tulikuwa na mafuriko makubwa hapa, ambayo hutokea kwa nadra. Ningependa kumwambia kila mtu aliye na kiu ya Mungu kile nilichokipitia kwa kweli na kukiona wakati huo.
Siku hiyo mume wangu nami tuliutunza uga wa chakula kikavu cha mifugo wa dada yangu. Wakati wa usiku mvua nzito iliendelea kunyesha, na tulienda kulala mapema sana. Saa nne kasorobo usiku ndugu mkwe wangu wa kiume aliita akisema: “Wanaelekea kufungua hodhi! Kila kitu kitafurikiwa!

Jumamosi, 25 Mei 2019

Wimbo wa Kuabudu | "Sifa kwa Maisha Mapya katika Ufalme" | Watu wa Mungu Humsifu na Kumwabudu Mungu



Wimbo wa Kuabudu | "Sifa kwa Maisha Mapya katika Ufalme" | Watu wa Mungu Humsifu na Kumwabudu Mungu

Tumesikia sauti ya Mungu na kurudi nyumbani Kwake. Mikutanoni tunakula na kunywa maneno ya Mungu, tunahudhuria karamu. Sisi tunaaga huzuni na vifungo vyetu, tunaishi maisha mapya. Maneno ya Mungu yako nasi kila siku, tunastarehe ndani yake. Tunapofungua mioyo yetu katika ushirika wa kweli, mioyo yetu inaangazwa sana. Tunatafakari, kufikiri maneno ya Mungu, Roho Mtakatifu anatuangazia. Tunaondolewa vizuizi na ubaguzi wetu, tunaishi ndani ya upendo wa Mungu.

Ijumaa, 24 Mei 2019

Mungu Aliilinda Familia Yetu Wakati wa Maafa

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Maafa

Mungu Aliilinda Familia Yetu Wakati wa Maafa

Agosti 6, Mwaka wa 2012
Mnamo Julai 21, mwaka wa 2012, mafuriko makubwa zaidi tangu miaka sitini yalipitia kijijini mwetu kwa nguvu mno. Maafa yalianguka kutoka mbinguni, maji ya mafuriko yalichanganya matope na mawe na kuharibu kijiji chote. Nyumba nyingi ziliharibiwa na maji na maporomoko ya matope.

Alhamisi, 23 Mei 2019

Umeme wa Mashariki | Katikati ya Maafa Niliiona Tabia ya Haki ya Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki, Maafa,
Li Jing, Beijing
7 Agosti, mwaka wa 2012
Siku hiyo, ilianza kunyesha asubuhi. Nilikwenda kwa mkutano nyumbani mwa ndugu mmoja, wakati mvua ilipoendelea kuongezeka zaidi na zaidi kwa uzito. Kufikia alasiri ilikuwa ikinyesha kana kwamba ilitoka mbinguni moja kwa moja. Wakati tulipomaliza mkutano wetu, mvua ilikuwa imeingia katika ua wa ndugu yangu, lakini kwa sababu nilikuwa na wasiwasi juu ya familia yangu, nilijitahidi kwenda nyumbani. Nusu ya barabara huko, baadhi ya watu waliokimbia hatari waliniambia, "Je, si wewe unatoroka, bado unakwenda nyumbani?" Nilipofika nyumbani, mtoto wangu aliniuliza, "Je, mafuriko hayakukuzoa?" Ni hapo tu nilipojua kwamba sikuwa na Mungu moyoni mwangu.

Jumatano, 22 Mei 2019

Kwa Kuelewea Hizi Hoja Nne, Uhusiano Wetu na Mungu Utakuwa Wa Karibu Daima

                              Na Xiaomo, China

Biblia inasema, “Kujeni karibu na Mungu, naye atakuja karibu nanyi” (Yakobo 4:8). Kama Wakristo, ni kwa kumkaribia Mungu tu na kuwa na ushirikiano halisi na Mungu ndiyo tunaweza kudumisha uhusiano wa kawaida na Mungu na kupata kazi ya Roho Mtakatifu. Ni kama tu watu wawili wanaoshirikiana, ambao wanaweza tu kuendeleza uhusiano wao wa karibu kwa muda mrefu kwa kuwa wazi zaidi kwa kila mmoja, kuwasiliana zaidi wanapokumbana na masuala, na kwa kuelewawana na kuheshimiana.

Jumanne, 21 Mei 2019

Baraka za Mungu: Huenda Nisiwe Tajiri, lakini Nina Bahati Sana


Nataka Kuwa Tajiri
“Mwalimu mkuu, tafadhali mpe mwanangu fursa na kumruhusu afanye mtihani!” Macho ya mama yangu yalimsihi mwalimu mkuu alipokuwa akizungumza kwa sauti ya kutetemeka kidogo.
Bila kuonyesha hisia, mwalimu mkuu akasema, “Hapana, shule ina kanuni. Mtoto anaweza kufanya mtihani tu wakati ada ya mtihani imelipwa!”