Jumanne, 25 Septemba 2018

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (3) - Je, Hakuna Maneno au Kazi ya Mungu Nje ya Biblia?

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (3) - Je, Hakuna Maneno au Kazi ya Mungu Nje ya Biblia?

Watu wengi katika ulimwengu wa kidini wanasadiki kwamba maneno yote ya Mungu yako ndani ya Biblia, na chochote kilicho nje ya Biblia hakina kazi Yake na maneno. Hawatafuti nje ya Biblia matamko Yake katika kurudi Kwake. Je, wataweza kukaribisha kurudi kwa Bwana kama wataendelea kushikilia wazo hili? Je, Mungu angeweza kuzuiliwa tu kwa kuongea maneno yaliyo ndani ya Biblia? Biblia inasema: "Na pia kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya, ambayo, yote yakiandikwa, ninafikiri kwamba hata dunia yenyewe haingetosha vitabu hivyo ambavyo vitaandikwa" (Yohana 21:25). Mungu anasema: "Yote yaliyoandikwa katika Biblia ni machache na hayawezi kuwakilisha kazi yote ya Mungu" (Neno Laonekana katika Mwili).

Tamko La Thelathini na Tatu

Tamko La Thelathini na Tatu

Ufalme Wangu unawahitaji wale ambao ni waaminifu, wasio wanafiki, na wasio wadanganyifu. Je, si watu wenye moyo safi na waaminifu duniani hawapendwi na watu? Mimi ni kinyume kabisa cha jinsi ilivyo. Inakubalika kwa watu waaminifu kuja Kwangu; Nafurahia mtu wa aina hii, pia Ninamhitaji mtu wa aina hii. Hii ni haki Yangu hasa. Watu wengine ni wajinga; hawawezi kuhisi kazi ya Roho Mtakatifu na hawawezi kuyaelewa mapenzi Yangu.

Jumatatu, 24 Septemba 2018

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (4) - Je, Kusamehewa kwa Dhambi Zetu Ndiko Kweli Tiketi kuelekea Ufalme wa Mbinguni?

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (4) - Je, Kusamehewa kwa Dhambi Zetu Ndiko Kweli Tiketi kuelekea Ufalme wa Mbinguni?

Watu wengi katika dini wanafikiria kuwa wamezikiri dhambi zao na kuzitubu baada ya kumsadiki Bwana, hivyo wamekombolewa, na wameokolewa kwa neema. Wakati Bwana atakapokuja, atawainua moja kwa moja hadi kwenye ufalme wa mbinguni, na haiwezekani Yeye kufanya kazi ya utakaso na wokovu. Je, mtazamo huu unalingana na uhalisi wa kazi ya Mungu? Inasemekana kwenye Biblia: "Utakatifu, bila huu hakuna mwanadamu atakayemwona Bwana" (Waebrania 12:14). Mungu anasema: "Umepitwa na hatua moja katika imani yako kwa Mungu: umekombolewa tu, lakini haujabadilishwa. Ili uipendeze nafsi ya Mungu, lazima Mungu Mwenyewe afanye kazi ya kukubadilisha na kukutakasa; ikiwa umekombolewa tu, hautakuwa na uwezo wa kufikia utakatifu. Kwa njia hii hautahitimu kushiriki katika baraka nzuri za Mungu" (Neno Laonekana katika Mwili).

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (5) - Je, Hukumu ya Mungu katika Siku za Mwisho ni Adhabu au Wokovu?

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (5) - Je, Hukumu ya Mungu katika Siku za Mwisho ni Adhabu au Wokovu?

Baadhi ya watu husoma maneno ya Mungu na kuona kwamba kunayo mambo makali ambayo ni hukumu ya wanadamu, na shutuma na laana. Wanafikiria kwamba kama Mungu huhukumu na kulaani watu, nao pia hawatashutumiwa na kuadhibiwa? Inawezaje kusemekana kwamba aina hii ya hukumu ni ya kutakasa na kuokoa wanadamu? Maneno ya Mungu yanasema: "Kile ambacho Mungu hulaani ni uasi wa mwanadamu, na kile Anachohukumu ni dhambi za mwanadamu." "Ufichuzi mkali wa neno ni kwa kusudi la kukuongoza kwenye njia sahihi" (Neno Laonekana katika Mwili). Ni njia gani nzuri ya kufahamu kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho?

Jumapili, 23 Septemba 2018

Tamko la Kumi na Mbili

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mungu, Umeme wa Mashariki

Tamko la Kumi na Mbili

Ikiwa una tabia ambayo si thabiti, nyepesi kuhamaki kama upepo au mvua, kama huwezi kuendelea kusonga mbele, basi fimbo Yangu haitakuwa mbali na wewe. Unaposhughulikiwa, kadiri hali ilivyo mbaya zaidi, na kadiri unavyoteswa zaidi, ndivyo upendo wako kwa Mungu unavyoongezeka, na unaacha kushikilia dunia. Bila njia nyingine, unakuja Kwangu, na unapata tena nguvu na imani yako. Ilhali, katika hali rahisi, ungeboronga. Ni lazima uingie ndani kwa mtazamo chanya, uwe mwenye vitendo na si baridi.

Swahili Christian Movie "Kutamani Sana" (4) - Je, Ufalme wa Mbinguni uko Mbinguni au Ulimwenguni?

Swahili Christian Movie "Kutamani Sana" (4) - Je, Ufalme wa Mbinguni uko Mbinguni au Ulimwenguni?

Watu wengi walio na imani kwa Bwana wanasadiki kwamba ufalme wa mbinguni uko mbinguni. Je, hivyo ndivyo ilivyo kwa kweli? Sala ya Bwana inasema: "Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe. Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni" (Mathayo 6:9-10). Kitabu cha Ufunuo kinasema, "Falme za dunia zimekuwa falme za Bwana wetu, na za Kristo wake" (Ufunuo 11:15). "Mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni, … maskani ya Mungu yako pamoja na wanadamu" (Ufunuo 21:2-3). Hivyo, ufalme wa mbinguni uko mbinguni au ulimwenguni?

Yaliyopendekezwa: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi MunguFilamu za Injili

Jumamosi, 22 Septemba 2018

Kuuonja Upendo wa Mungu Katikati ya Dhiki



Kanisa la Mwenyezi Mungu, kanisa, Umeme wa Mashariki

93. Kuuonja Upendo wa Mungu Katikati ya Dhiki

Chen Lu Wilaya ya Tonglu, Mkoa wa Zhejiang
Nilizaliwa miaka ya 1980 katika kijiji—tulikuwa tumekuwa familia ya wakulima kwa vizazi vingi. Nilijiingiza katika masomo yangu ili niweze kuhitimu kuingia katika chuo na kuepuka maisha ya kijijini ya umasikini na hali ya kuwa nyuma. Nilipoanza shule ya upili, nilikutana na Historia ya Sanaa ya Magharibi, na wakati nilipoona picha nyingi za kupendeza kama vile "Mwanzo," "Bustani ya Edeni," na "Mlo wa Mwisho," ni hapo tu nilipojua kwamba kulikuwa na Mungu katika ulimwengu aliyeumba vitu vyote. Sikuweza kujizuia kuwa na moyo uliojaa hamu ya Mungu. Baada ya kuhitimu kutoka chuo, nilipata kazi nzuri kwa urahisi sana, na kisha nikampata patna mzuri. Hatimaye nilikuwa nimefanikisha matarajio yangu mwenyewe na yale ya mababu zangu. Nilikuwa nimeepuka nasaba ya mababu zangu ya kuuweka uso wao chini na mgongo kuangalia mbinguni, na mwaka wa 2008, kuzaliwa kwa mtoto kuliongeza furaha zaidi kwa maisha yangu. Nikiangalia kila kitu nilichokuwa nacho katika maisha yangu, niliamini kuwa nilistahili niwe na maisha ya furaha, ya kustarehesha.