Jumamosi, 25 Mei 2019

Wimbo wa Kuabudu | "Sifa kwa Maisha Mapya katika Ufalme" | Watu wa Mungu Humsifu na Kumwabudu Mungu



Wimbo wa Kuabudu | "Sifa kwa Maisha Mapya katika Ufalme" | Watu wa Mungu Humsifu na Kumwabudu Mungu

Tumesikia sauti ya Mungu na kurudi nyumbani Kwake. Mikutanoni tunakula na kunywa maneno ya Mungu, tunahudhuria karamu. Sisi tunaaga huzuni na vifungo vyetu, tunaishi maisha mapya. Maneno ya Mungu yako nasi kila siku, tunastarehe ndani yake. Tunapofungua mioyo yetu katika ushirika wa kweli, mioyo yetu inaangazwa sana. Tunatafakari, kufikiri maneno ya Mungu, Roho Mtakatifu anatuangazia. Tunaondolewa vizuizi na ubaguzi wetu, tunaishi ndani ya upendo wa Mungu.

Ijumaa, 24 Mei 2019

Mungu Aliilinda Familia Yetu Wakati wa Maafa

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Maafa

Mungu Aliilinda Familia Yetu Wakati wa Maafa

Agosti 6, Mwaka wa 2012
Mnamo Julai 21, mwaka wa 2012, mafuriko makubwa zaidi tangu miaka sitini yalipitia kijijini mwetu kwa nguvu mno. Maafa yalianguka kutoka mbinguni, maji ya mafuriko yalichanganya matope na mawe na kuharibu kijiji chote. Nyumba nyingi ziliharibiwa na maji na maporomoko ya matope.

Alhamisi, 23 Mei 2019

Umeme wa Mashariki | Katikati ya Maafa Niliiona Tabia ya Haki ya Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki, Maafa,
Li Jing, Beijing
7 Agosti, mwaka wa 2012
Siku hiyo, ilianza kunyesha asubuhi. Nilikwenda kwa mkutano nyumbani mwa ndugu mmoja, wakati mvua ilipoendelea kuongezeka zaidi na zaidi kwa uzito. Kufikia alasiri ilikuwa ikinyesha kana kwamba ilitoka mbinguni moja kwa moja. Wakati tulipomaliza mkutano wetu, mvua ilikuwa imeingia katika ua wa ndugu yangu, lakini kwa sababu nilikuwa na wasiwasi juu ya familia yangu, nilijitahidi kwenda nyumbani. Nusu ya barabara huko, baadhi ya watu waliokimbia hatari waliniambia, "Je, si wewe unatoroka, bado unakwenda nyumbani?" Nilipofika nyumbani, mtoto wangu aliniuliza, "Je, mafuriko hayakukuzoa?" Ni hapo tu nilipojua kwamba sikuwa na Mungu moyoni mwangu.

Jumatano, 22 Mei 2019

Kwa Kuelewea Hizi Hoja Nne, Uhusiano Wetu na Mungu Utakuwa Wa Karibu Daima

                              Na Xiaomo, China

Biblia inasema, “Kujeni karibu na Mungu, naye atakuja karibu nanyi” (Yakobo 4:8). Kama Wakristo, ni kwa kumkaribia Mungu tu na kuwa na ushirikiano halisi na Mungu ndiyo tunaweza kudumisha uhusiano wa kawaida na Mungu na kupata kazi ya Roho Mtakatifu. Ni kama tu watu wawili wanaoshirikiana, ambao wanaweza tu kuendeleza uhusiano wao wa karibu kwa muda mrefu kwa kuwa wazi zaidi kwa kila mmoja, kuwasiliana zaidi wanapokumbana na masuala, na kwa kuelewawana na kuheshimiana.

Jumanne, 21 Mei 2019

Baraka za Mungu: Huenda Nisiwe Tajiri, lakini Nina Bahati Sana


Nataka Kuwa Tajiri
“Mwalimu mkuu, tafadhali mpe mwanangu fursa na kumruhusu afanye mtihani!” Macho ya mama yangu yalimsihi mwalimu mkuu alipokuwa akizungumza kwa sauti ya kutetemeka kidogo.
Bila kuonyesha hisia, mwalimu mkuu akasema, “Hapana, shule ina kanuni. Mtoto anaweza kufanya mtihani tu wakati ada ya mtihani imelipwa!”

Jumatatu, 20 Mei 2019

Kwaheri kwa Zile Siku za Kushindana na Majaliwa

Smiley face

Kijiji cha kishamba kilichojikokota kimaendeleo, wazazi wangu waliochoka kwa sababu ya kazi zao, maisha ya shida za kifedha … kumbukumbu hizi za huzuni zilitia alama kwa mawazo yangu machanga, zilikuwa ni hisia yangu ya kwanza ya “majaliwa.” Baada ya kuanza kwenda shule, mara ya kwanza nilipomsikia mwalimu wangu akisema kwamba “Unadhibiti majaliwa yako katika mikono yako mwenyewe,” niliweka maneno haya imara mawazoni mwangu.

Jumapili, 19 Mei 2019

Neno la Mungu | “Mwanadamu Mpotovu Hawezi Kumwakilisha Mungu”


Neno la Mungu | “Mwanadamu Mpotovu Hawezi Kumwakilisha Mungu”

Mwenyezi Mungu anasema, “Vitendo vyote na matendo ya Shetani vinaonyeshwa kupitia kwa binadamu. Sasa vitendo vyote na matendo yote ya binadamu ni maonyesho ya Shetani na hivyo basi haviwezi kumwakilisha Mungu. Binadamu ni mfano halisi wa Shetani, na tabia ya mwanadamu haiwezi kuiwakilisha tabia ya Mungu. Baadhi ya wanadamu ni wenye tabia nzuri; Mungu anaweza kufanya baadhi ya kazi kupitia kwa tabia hiyo nayo kazi yao inatawaliwa na Roho Mtakatifu. Ilhali tabia yao haiwezi kumwakilisha Mungu. Kazi ambayo Mungu hufanya ndani yao ni kule tu kufanya kazi na pamoja na kupanua kile ambacho tayari kimo ndani yao. Wawe ni manabii au binadamu wanaotumiwa na Mungu kutoka kwa enzi zilizopita, hakuna yeyote anayeweza kumwakilisha Mungu moja kwa moja.” “Kwani kiini cha binadamu ni tofauti na kile cha Mungu. Binadamu hawezi kamwe kuishi kwa kumdhihirisha Mungu, sembuse kuwa Mungu. Kile ambacho Roho Mtakatifu anamwelekeza binadamu kuishi kwa kudhihirisha ni kulingana tu na kile ambacho Mungu anahitaji kutoka kwa binadamu.”

Tazama zaidi: Maonyesho ya Mungu | "Mwanadamu Anaweza Kuokolewa tu Katikati ya Usimamizi wa Mungu"

Kujua zaidi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?